Monday, 3 September 2018

Michezo

Mfahamu kocha wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Emmanuel Amunike



Amunuke ni nani?
Alizaliwa mwaka 1970 katika Mji wa Eziobodo nchini Nigeria
Alianza soka la ushindani mwaka 1990 kwa kuichezea timu ya Concord na Julius Berger zote za Nigeria.
Mwaka 1991 hadi 1994 aliitumikia Zamalek ya Misri kabla kujiunga na Sporting Lisbon ya Ureno kutoka mwaka 1994 hadi 1996.
Amunike pia aliitumikia Barcelona ya Hispania kutoka mwaka 1996 hadi mwaka 2000.
Klabu nyingine alizowahi kuzitumikia enzi za uchezaji wake ni Albacete ya Hispania,Busan I’cons na Al-Wehdat.
Amunike pia aliitumikia timu ya Taifa ya Nigeria kwa miaka minane, na alikuwemo kwenye kikosi kilichoshiriki fainali za Kombe la dunia mwaka 1994 nchini Marekani.
Historia yake katika ufundishaji soka inabainisha kuanza miama kumi iliyopita ambapo amezinoa klabu mbalimbali zikiwemo Julius Berger, Al Hazm,Ocean Boys,Timu ya Vijana ya Nigeria chini ya miaka 17 na Klabu ya Al-Khartoum y Sudan.

No comments: