Nchi za Afrika zimeonyesha hamu kubwa kwa mikopo ya China lakini baadhi ya wataalamu sasa wana hofu kuwa bara la Afrika huenda likajikuta kwenye madeni makubwa.
Barabara ya Entebbe-Kampala inaweza kutajwa kuwa kuvutio cha watalii kwa watu nchini Unganda karibu miezi mitatu tangu izinduliwe.
Barabara hiyo ya umbali wa kilomita 51 inayounganisha mji mkuu Kampala kwenda uwanja wa ndege wa kimataifa wa Entebe, ilijengwa na kampuni ya Kichina kwa gharama ya dola milioni 476 kutoka mkopo wa China Exim BANK.

No comments:
Post a Comment